RAIS KENYATA AIDHINISHA SHERIA ZA UHALIFU WA KOMPYUTA.


Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ameidhinisha Mswada wa Sheria za Uhalifu wa Kompyuta na Mtandaoni wa 2018 kuwa Sheria, hatua itakayotoa adhabu kali kwa watakaopatikana na makossa ya mtandaoni.
Image result for PICHA KENYATTA
RAIS KENYATA
Sheria hiyo inatoa adhabu ya faini ya Shilingi milioni 5 ya Kenya sawa dola elfu hamsini za Marekani au kifungo cha miaka miwili jela, au adhabu zote mbili, kwa atakayepatikana na kosa la uenezaji wa habari za uzushi.
Pia mswada huo wa sheria unaeleza kuwa mtu atakayepatikana na kosa la kueneza taarifa ambazo zinaweza kuzua taharuki au vurugu atafungwa jela zaidi ya miaka kumi.

Baadhi ya wadau wanasema kuwa sheria hiyo inatarajiwa kuathiri utendaji kazi wa wanahabari, vyombo vya habari, watumiaji wa mitandao ya kijamii, wanavitalu na watu wengine wanaotumia kompyuta na mitandao.

Kiongozi wa zamani wa Chama cha Wanasheria Kenya Apollo Mboya amenukuliwa na vyombo vya habari akisema kifungu hicho kinaweza kuwapa watawala,uhuru wa kukandamiza vyombo vya habari.



RAIS KENYATA AIDHINISHA SHERIA ZA UHALIFU WA KOMPYUTA. RAIS KENYATA AIDHINISHA SHERIA ZA UHALIFU WA KOMPYUTA. Reviewed by safina radio on May 16, 2018 Rating: 5

No comments