SERIAKALI KUENDELEA KUBORESHA VITUO VYA AFYA HAPA NCHINI.


 Serikali imesema kuwa inaendelea kuboresha na kumalizia ujenzi wa vituo vya afya 208 kote nchini ili kuboresha utoaji wa huduma za afya karibu na wananchi kwa lengo la kuwapunguzia changamoto za kufuata huduma hizo umbali mrefu.

Image result for PICHA YA JOSEPHAT KAKUNDA
MH. KAKUNDA

Hayo yamesemwa leo bungeni jijini Dodoma na naibu waziri ofisi ya Rais tawala za mikoa na serikali za mitaa Tamisemi Mh. Joseph Kakunda wakati akijibu swali la mbunge wa Rungwe Mh Saul Henry Amon aliyetaka kujua ni lini serikali itamalizia vituo vya afya ambavyo bado ujenzi wake haujakamilika.

Mh Kakunda amesema kuwa katika halmashauri ya wilaya ya Rungwe serikali imepeleka shilingi bilioni moja ambapo mwezi septemba mwaka 2017 serikali ilipeleka shilingi milioni mia tano kwenye kituo cha afya cha Ikuti kwa ajili ya ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje OPD,chumba cha upasuaji,wodi ya watoto na wodi ya mama wajawazito.
                                         

Wakati huo huo serikali imesema kuwa katika mwaka wa fedha 2018/2019 imetenga fedha kiasi cha shilingi bilioni 1.2 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji vijijini katika halmashauri ya wilaya ya Monduli.

Image result for PICHA YA JUMA AWESO NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI
MH. AWESO
Hayo yamesemwa na naibu waziri wa maji na umwagiliaji Mh. Juma Aweso  wakati akijibu swali la mbunge wa Monduli Mh. Julius Kalanga laizer aliyetaka kujua ni lini serikali itatimiza ahadi ya rais ya ukarabati ya mabwawa matatu wilayani Monduli.
                                      


SERIAKALI KUENDELEA KUBORESHA VITUO VYA AFYA HAPA NCHINI. SERIAKALI KUENDELEA KUBORESHA VITUO VYA AFYA HAPA NCHINI. Reviewed by safina radio on May 15, 2018 Rating: 5

No comments