WAZIRI JAFFO AKATAA GHARAMA ZA UJENZI WA BWENI.
Waziri wa nchi ofisi ya Rais tawala za
mikoa na serikali za mitaa Tamisemi Mh.
Selemani Jaffo amesema hajaridhishwa na mradi wa ujenzi wa bweni la shule ya
Endasak wilayani Hanang mkoani Manyara kutokana na matumizi ya fedha kiasi cha
shilingi milioni 170.6
Waziri Jaffo ameeleza kutoridhishwa kwake
na mradi huo kwani halmashauri nyingine zinatumia fedha kiasi cha shilingi
milioni mia moja na hamsini kujenga mabweni mawili.
Hata hivyo waziri Jaffo akizungumza na wanafunzi
wa shule ya sekondari ya Endasak amesema kuwa serikali ina mpango wa kuongeza
shule za sekondari wilayani Hanang.
Awali akitoa taarifa ya utekelezaji wa
mradi mradi huo Mwalimu Gisela Msofe amesema kuwa mradi huo wa bweni lenye
vyumba ishirini litakalo chukua wanafunzi 80 umefadhiliwa na taasisi ya elimu TEA.
WAZIRI JAFFO AKATAA GHARAMA ZA UJENZI WA BWENI.
Reviewed by safina radio
on
May 16, 2018
Rating:
No comments