KAMPUNI 37 ZASHINDA ZABUNI KWA KUSAINI MIKATABA 50 ZA UJENZI WA BARABARA, HALMASHAURI 9 MKOANI MTWARA.


MTWARA.



Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini-TARURA mkoani Mtwara imesaini mikataba 50 na kampuni 37 zilizoshinda zabuni ya kujenga Barabara katika Halmashauri 9 mkoani humo.

Mratibu wa TARURA mkoa wa Mtwara Mhandisi Seraji Mvuta amesema miradi ya ujenzi wa barabara hizo zitakazogharimu fedha jumla ya shilingi bilioni 4 unatarajiwa kukamilika ndani ya mwaka huu wa fedha 2017/2018.

Aidha, Mhandisi Mvuta amesema kuwa lengo la kutekeleza mradi huo katika kipindi cha mwaka huu wa fedha 2017/2018 ni kuhakikisha kuwa wanapanga kutekeleza miradi mingine katika mwaka wa fedha ujao.

Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi Mkoani humo Bw Elias Majisani amezitaka kampuni zilizoshinda zabuni ya ujenzi wa barabara kutoa fursa za ajira kwa wakazi wa maeneo husika wakati wa utekelezaji wa miradi hiyo ili nao waweze kunufaika.

Amesema kuwa hategemei kuona kuwa Mkandarasi anawachukua vibarua katika mikoa ya Lindi au Mtwara mjini kuwapeleka Tandahimba wakati kuna watu katika maeneo hayo wanaweza kufanya kazi za kawaida ambazo hazihitaji mtu kuwa na taaluma.


KAMPUNI 37 ZASHINDA ZABUNI KWA KUSAINI MIKATABA 50 ZA UJENZI WA BARABARA, HALMASHAURI 9 MKOANI MTWARA. KAMPUNI 37 ZASHINDA ZABUNI KWA KUSAINI MIKATABA 50 ZA UJENZI WA BARABARA, HALMASHAURI 9 MKOANI MTWARA. Reviewed by safina radio on February 16, 2018 Rating: 5

No comments