Naibu Waziri wa Madini Mh. Doto Biteko amesema kuwa serikali inaendelea kuwawazesha wachimbaji wadogo wa madini vifaa kupitia ruzuku ya wachimbaji badala ya kutoa fedha taslim ambazo zimekuwa zikiombwa na wachibaji wasiokuwa na sifa.
KATAVI.
Naibu Waziri wa Madini Mh. Doto Biteko amesema kuwa
serikali inaendelea kuwawazesha wachimbaji wadogo wa madini vifaa kupitia
ruzuku ya wachimbaji badala ya kutoa fedha taslim ambazo zimekuwa zikiombwa na
wachibaji wasiokuwa na sifa.
Naibu Waziri Biteko ameyasema hayo katika mkutano wa
hadhara katika eneo la machimbo ya Kapanda Wilayani Mpanda akiwa katika ziara ya siku moja ya kuangalia
shughuli za wachimabaji katika mkoa wa Katavi.
Aidha amebainisha kuwa fedha hizo za ruzuku
zilizotolewa zinauwezekano wa kuwa zimetolewa kwa wachimbaji wasio wadogo bali
kwa watu wachache wanaojua kuwasilisha masuala yao pamoja na kuwa na mtandao hadi
ofisi za wizara.
Pia, amesema kuwa kuna viongozi ambao wanachukua
fedha kutoka kwa watu hao takribani dola elfu hamsini hadi laki moja ambapo baada
ya kupata fedha hizo walikwenda kufungulia biashara zao.
Hali kadhalika Mh. Biteko amesema kuwa kuna kiongozi
ambaye amepatiwa fedha kiasi cha dola elfu hamsini sawa na shilingi milioni mia
moja za Kitanzania na kuifanyia biashara kwa kununua ng’ombe na kusafirisha
kwenda Dar es salaam kwa malori.
Awali akisoma risala,Katibu wa Wachimbaji wadogo wa
madini kwa Mkoa wa Katavi Silibeti Sanga ameiomba serikali kuendelea kuwasaidia
wachimbaji wadogo,kauli iliyoungwa mkono na Mwenyekiti wake Willium Mbogo.
Naibu Waziri wa Madini Mh. Doto Biteko amesema kuwa serikali inaendelea kuwawazesha wachimbaji wadogo wa madini vifaa kupitia ruzuku ya wachimbaji badala ya kutoa fedha taslim ambazo zimekuwa zikiombwa na wachibaji wasiokuwa na sifa.
Reviewed by safina radio
on
February 26, 2018
Rating:

No comments