DK. SLAA NA MUHIDINI WAMEAPISHWA LEOKUWA MABALOZI WA SWEDEN NS NIGERIA. JIJINI DAR ES SALAAM.
DAR-ES-SALAAM.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mh. Dk John Magufuli leo amewaapisha Mabalozi wawili watakaowakilisha
Tanzania katika nchi za Sweeden na Nigeria.
Hafla ya kuapishwa kwa mabalozi hao imefanyika
Ikulu jijini Dar es salaam ambapo mabalozi walioapishwa ni pamoja na Dk.
Wilbrod Peter Slaa ambaye anakuwa balozi wa Tanzania nchini Sweeden na Muhidi Ally Muhoto anayekwenda
nchini Nigeria.
![]() |
Dk, Wilrod Peter Slaa.amekuwa Balozi wa Tanzania nchni Sweden. |
![]() |
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dk. Suzan Alphonce Kolimba akieleza jambo kwa mabalozi wapya. |
Hata hivyo mara baada ya kuapishwa kwa
mabalozi hao pia walikula kiapo cha Uadilifu kwa Viongozi wa Umma kinachotolewa
na Kamishna wa Maadili hapa nchini Jaji Mstaafu Harold Reginald Nsekela huku mabalozi hao wakiahidi kutoa ushirikiano kwa serikali na
kutekeleza viapo vyao walivyoapa.
![]() |
Mabalozi wapya wakila kiapo mbele ya rais wa Tanzania. |
DK. SLAA NA MUHIDINI WAMEAPISHWA LEOKUWA MABALOZI WA SWEDEN NS NIGERIA. JIJINI DAR ES SALAAM.
Reviewed by safina radio
on
February 16, 2018
Rating:

No comments