LUTEN JENERALI YAKUBU HASSAN MOHAMED AAPISHWA KUWA MNADHIMU MKUU WA JESHI LA JWTZ.


DAR-ES-SALAAM.

Taarifa ya Habari 01:00 mchana, 15 February, 2018.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mh. Dk. John Magufuli amemuapisha Luteni Jenerali Yakubu Hassan Mohamed kuwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania-JWTZ.

Hafla hiyo iliyofanyika leo Ikulu jijini Dr es salaam pia imetanguliwa kwa kupandishwa vyeo kwa takriban Mabrigedia Jenerali kumi kutoka cheo cha Brigedia Jenerali kuwa Meja Jenerali katika jeshi hilo.  

Aidha, baada ya Rais Magufuli kuridhia  pendekezo la Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, JeneraliVenance Mabeho, amewapandisha vyeo, Meja Jenerali Jacob Gidion Pingu kuwa katika kommandi  NDC na Meja Jenerali Shilinyi Msungu kuwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa-JKT, kufuatia nafasi hizo kuwa wazi.

Vile vile, Jenerali Mabeho, ametaja kuwapo kwa mabadiliko katika baadhi ya vitengo vya jeshi zikiwemo za Mkuu wa Mafunzo Jeshini, Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu, Kamandi ya vikosi chini ya Makao Makuu ya Jeshi, huku akiwapandisha wakuu wa vitengo vya ukurugenzi, na Msimamizi Mkuu wa Jeshi.

Kwa upande wake Waziri wa jeshi la ulinzi na usalama nchini Hussen Ally Mwinyi, amepongeza kuapishwa kwa Luteni Jenerali Yakubu Hassan Mohamed na kupandishwa vyeo kwa Mabrigedia Jenerali Kumi kuwa Mameja Jenerali , huku akielezea sifa za Jeshi la Wananchi wa Tanzania-JWTZ,kuwa jeshi lenye linalofaa kuigwa katika bara la Afrika na Duniani kutokana na nidhamu ya jeshi hilo.

Hata  hivyo  Luteni Jenerali Yakubu Hassan Mohamed amechukua nafasi  hiyo iliyokuwa  inashikiliwa na  Luteni Jenerali James Aloice Mwakibolwa  baada  ya  kustaafu kwake .


LUTEN JENERALI YAKUBU HASSAN MOHAMED AAPISHWA KUWA MNADHIMU MKUU WA JESHI LA JWTZ. LUTEN JENERALI YAKUBU HASSAN MOHAMED AAPISHWA KUWA MNADHIMU MKUU WA JESHI LA JWTZ. Reviewed by safina radio on February 15, 2018 Rating: 5

No comments