HALMASHAURIYA WILAYA YA SHINANGA IMEKAMILISHA JENGO LA WAGONJWA WA NJE YAANI OPD.


TAREHE 09-02-2018
Image result for PICHA NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI JOSEPHAT KANDEGE AKIWA BUNGENI


Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kupitia fedha za ruzuku kutoka serikali imekamilisha ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje yaani OPD na nyumba moja ya watumishi pamoja na jengo lakutolea huduma ya ushauri nasaha ambalo liko katika hatua za upauaji.

Hayo yamesemwa na Naibu waziri wa ofisi ya rais tawala za mikoa na serkali za mitaa-TAMISEMI Josephat Kandege wakati akijibu swali la Aza Hilal Hamad mbunge wa viti maalumu aliyehoji kuwa serikali itapeleka lini fedha za kutosha kukamilisha ujenzi wa hospitali ya wilaya ya shinyanga ambao umeamzishwa kwa nguvu za wananchi katika mkutano wa kumi wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linaloendelea mjini Dodoma.

Aidha, Mh. Kandege amesema Jumla ya kiasi cha fedha shilingi milioni mia tatu sitini na tano zilitumika kutoka katika vyanzo mbali mbali ambazo ni kiasi cha shilingi milioni mia mbili sitini na saba ruzuku kutoka serikali kuu, mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya shilingi milioni themanini na sita, nguvu za wananchi shilingi milioni saba na mchango wa rais mstaafuu wa awamu ya nne Dk. Jakaya Kikwete shilingi miliolni tano.

Katika mwaka wa fedha 2017/2018 zimetengwa silingi milioni mia moja na kumi kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa hospitali hiyo ambapo kati ya fedha hizo shilingi milioni arubaini ni mapato ya ndani ya halmashauri na shilingi milioni sabini ni ruzuku kutoka serikali kuu.

Hali kadhalika kwa mwaka wa fedha 2018/2019 zimetengwa shilingi milioni mia moja na kumi kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa hospitali hiyo ambapo shilingi milioni hamsini ni mapato ya ndani ya halamshauri ya wilaya na shilingi milioni sitini ni ruzuku kutoka serikali kuu.

Hata hivyo serikali itaendelea na ujenzi wa hospitali hiyo kulingana na upatikanaji wa fedha ili wananchi waweze kupata huduma.

HALMASHAURIYA WILAYA YA SHINANGA IMEKAMILISHA JENGO LA WAGONJWA WA NJE YAANI OPD. HALMASHAURIYA WILAYA YA SHINANGA IMEKAMILISHA JENGO LA WAGONJWA WA NJE YAANI OPD. Reviewed by safina radio on February 09, 2018 Rating: 5

No comments