Mawaziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya wamesema huenda umoja huo ukaiwekea Cam bodia vikwazo ikiwa nchi hiyo haitasitisha hujuma dhidi ya demokrasia na utawala wa kisheria.


BRUSSELS.

Mawaziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya wamesema huenda umoja huo ukaiwekea Cam bodia vikwazo ikiwa nchi hiyo haitasitisha hujuma dhidi ya demokrasia na utawala wa kisheria.
Mkuu wa sera za nje wa Umoja wa Ulaya Federica Mogherini (Kushoto) akisalimiana na waziri wa Mambo ya nchi za nje wa Uhispania, Jose Manuel Garcia-Margallo mjini Brussels

Mawaziri hao wameonya kuhusu hali ya kutisha ya kudorora kwa demokrasia, heshima kwa haki za binadamu na utawala wa sheria pamoja na kuongezeka kwa ukandamizaji wa wapinzani, vyombo vya habari na wanaharakati nchini Cam bodia.

Mawaziri hao wameihimiza nchi hiyo kurejesha demokrasia na wameitaka serikali kuwashirikisha viongozi waliochaguliwa katika mazungumzo muhimu, baada ya chama kikuu cha upinzani kuvunjwa kwa lazima mwezi Novemba mwaka uliopita.

 Umoja wa Ulaya pia umeelezea wasiwasi wake kwa hatua ya kukamatwa kwa kiongozi wa upinzani wa Cam bodia Kem Sokha, na imeishauri Cam bodia kukoma kutumia mahakama kama kifaa cha kisiasa kuwahangaisha wanasiasa wa upinzani na wanaharakati wengine.


Mawaziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya wamesema huenda umoja huo ukaiwekea Cam bodia vikwazo ikiwa nchi hiyo haitasitisha hujuma dhidi ya demokrasia na utawala wa kisheria. Mawaziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya wamesema huenda umoja huo ukaiwekea Cam bodia vikwazo ikiwa nchi hiyo haitasitisha hujuma dhidi ya demokrasia na utawala wa kisheria. Reviewed by safina radio on February 26, 2018 Rating: 5

No comments