WAZIRI LUKUVI AMEZITAKA HALMASHAURI ZOTE KUKAMILISHA ZOEZI LZA UKUSANYAJI KODI YA ARDHI IFIKAPO APRILI 30 MWAKA HUU

TAREHE 20-02-2018



Halmashauri  za  wilaya  na   manispaa  kote  nchini zimetakiwa  kukamilisha  zoezi  la  ukusanyaji  kodi  ya  ardhi   kwa  asilimia  miamoja   hadi  ifikapo   aprili  30   mwaka  huu kabla  ya  serikali  kuzichukulia  hatua  halmashauri  zitakazoshindwa  kutekeleza  agizo  hilo  .

 Kauli hiyo imetolewa na Waziri  wa  ardhi na maendeleo  ya  nyumba  na  makazi   Mh.  Wiliam  Lukuvi   katika  kikao  cha  watendaji  wa  idara  ya  ardhi  wilayani  Bukoba   mkoani  Kagera  alipokuwa  katika  ziara  yake   ya  kikazi  mkoani  humo.

Mh,Lukuvi  amelazimika kutoa  kauli  hiyo  kufuatia   kusikitishwa  kwake  na  hali  ya  ukusanyaji  wa  kodi  kwa  baadhi  ya  idara  za  ardhi  hapa  nchini  ikiwemo  wilaya  Bukoba   ambayo  kwa  mwaka  wa  fedha   wa  serikali  2017/2018  Imeshindwa  kufikia  malengo  ya ukusanyaji wa  kodi  ya  ardhi  kwa  asilimia mia moja  kama  ilivyojipangia 

Amesema kuwa Halmashauri  ya  wilaya  ya  Bukoba  ilikusanya  kodi  ya   shilingi milioni  100   kati  ya  milioni  500   zilizopaswa  kukusanywa  2017/2018  makusanyo  ambayo   Mh,waziri  aliyaona  ni   hafifu  kulingana  na  malengo  yaliyowekwa  .

Hata  hivyo  imebainika  kuwepo  kwa  baadhi  ya  halmashauri ambazo   zimewamilikishia  watu  ardhi  kwa  kuwarasimisha  huku  ardhi  zenyewe  zikiwa  hazijapimwa  kisheria  hali  ambayo  huisabishia serikali  hasara  ama  kutoa  mwanya  kwa  wanyonge  kuonewa  na  baadhi  ya watu   wenye dhamana  na  matajiri 

WAZIRI LUKUVI AMEZITAKA HALMASHAURI ZOTE KUKAMILISHA ZOEZI LZA UKUSANYAJI KODI YA ARDHI IFIKAPO APRILI 30 MWAKA HUU WAZIRI LUKUVI AMEZITAKA HALMASHAURI ZOTE KUKAMILISHA ZOEZI LZA UKUSANYAJI KODI YA ARDHI IFIKAPO APRILI 30 MWAKA HUU Reviewed by safina radio on February 20, 2018 Rating: 5

No comments