Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Dk. John Pombe Maguli hii leo amehudhuria Mkutano wa 19 wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki mjini Kampala nchini Uganda.


KAMPALA.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Dk. John Pombe Maguli hii leo amehudhuria Mkutano wa 19 wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki mjini Kampala nchini Uganda.



Akizungumza wakati wa Mkutano huo Rais Magufuli ametoa wito kwa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Makatibu Wakuu na Mawaziri wa Jumuiya hiyo kuwa kubadilisha mawazo yao ili fedha wanazokusanya ndani ya nchi zao kwa ziweze  kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Aidha, Rais Magufuli amesema kuwa kutokana na tafiti zilizofanywa na Jopo la Nchi za Afrika linaloongozwa na Rais Mstaafu wa Afrika Kusini Tabo Mbeki inaeleza kuwa nchi za Afrika zinapoteza wastani wa dola bilioni 150 kila mwaka kutokana na utoroshaji wa rasilimali nje ya nchi.

Amesema kuwa Tanzania kwa sasa imeanza  kukusanya mapato ya ndani kutoka vyanzo mbalimbali vya mapato yanayofanikisha  ujenzi wa treni ya kisasa itakayogharimu kiasi cha dola za marekeani bilioni 3.5.

Hata hivyo, Mkutano huo wa wakuu wa nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki umelenga  kurejelea mikutano ya nyuma iliyofanyika mwaka 2004, 2012, na 2014 na kutoa msaada wa msukumo wa kisiasa katika kuunganisha mchakato wa agenda katika ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ili kutekeleza mipango ya kimaendeleo.
 Mkutano huo pia umehudhuriwa na Wakuu wa Nchi za Jumaiya ya Afrika Mashariki ambao ni Rais Kaguta Museven wa Uganda, Uhuru Kenyata wa Kenya, na Salva Kir wa Sudani Kusini, huku wakuu wa nchi za Rwanda na Burundi wakiwa wametuma wawakilishi wao.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Dk. John Pombe Maguli hii leo amehudhuria Mkutano wa 19 wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki mjini Kampala nchini Uganda. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Dk. John Pombe Maguli hii leo amehudhuria Mkutano wa 19 wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki mjini Kampala nchini Uganda. Reviewed by safina radio on February 22, 2018 Rating: 5

No comments