Mahakama nchini Iraq imewahukumu adhabu ya kifo wanawake 16 wa Kituruki waliokutwa na hatia ya kuwa Wanachama wa kundi la kigaidi linalojiita Dola la Kiislam-IS.



BAGDAD.

Mahakama  nchini Iraq imewahukumu adhabu ya kifo wanawake 16 wa Kituruki waliokutwa na hatia ya kuwa Wanachama wa kundi la kigaidi linalojiita Dola la Kiislam-IS.

Baadhi ya wanawake kutoka nchini Uturuki walishtakiwa nchini Iraq
Baadhi ya wanawake hao wenye umri wa miaka 20 hadi 50, waliingia Iraq  na watoto wadogo ambapo Wanawake hao waliiambia mahakama kwamba waliingia nchini Iraq kinyume na sheria kuwafuata waume zao ambao ni wanamgambo wa kundi la IS.

Iraq imeshawakamata wanawake 560 na watoto 600 wanaodaiwa kuwa na uhusiano na kundi la IS, na imeharakisha  kuwafungulia mashtaka.

Shirika la Kimataifa la Kutetea Haki za Binaadamu, Human Rights Watch limesema hukumu hiyo si ya haki, huku baadhi ya wanaharakati wakihoji kwamba wengi wao walidanganywa au kulazimishwa kujiunga na kundi hilo la kigaidi.

Mahakama nchini Iraq imewahukumu adhabu ya kifo wanawake 16 wa Kituruki waliokutwa na hatia ya kuwa Wanachama wa kundi la kigaidi linalojiita Dola la Kiislam-IS. Mahakama  nchini Iraq imewahukumu adhabu ya kifo wanawake 16 wa Kituruki waliokutwa na hatia ya kuwa Wanachama wa kundi la kigaidi linalojiita Dola la Kiislam-IS. Reviewed by safina radio on February 26, 2018 Rating: 5

No comments