ZUMA APEWA SIKU MBILI NA CHAMA CHAKE KUACHIA NGAZI
TAREHE 13-02-2018
Chama tawala nchini Afrika Kusini cha
African National Congress, ANC kimemtaka Rais Jacob Zuma kuachia madaraka kama
kiongozi wa taifa hilo.
Ripoti kutoka ndani ya kamati kuu ya chama hicho
zimesema kwamba Zuma amepewa siku mbili za kujiuzulu.
Hatua hii inatokea baada
ya kikao kilichodumu kwa muda wa saa 13 na kuhusisha viongozi wa juu wa chama.
Rais Jacob Zuma ametakiwa kuachia
madaraka na chama chake mwenyewe cha ANC mapema hii leo, kufuatia wiki moja ya
minong'ono kuhusiana na hatma ya uongozi wake.
Iwapo atagoma kujiuzulu anaweza kukabiliwa na
kura ya bunge ya kutokuwa na imani naye, wakati ambapo tayari tarehe ya kura
hiyo ilikwishapangwa kuwa ni Februari 22.
ZUMA APEWA SIKU MBILI NA CHAMA CHAKE KUACHIA NGAZI
Reviewed by safina radio
on
February 13, 2018
Rating:

No comments