CHOI SOON SIL, AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MAISHA KWA KASHFA ZA RUSHWA.


SEOUL

Taarifa ya Habari saa 08:00 usiku, 13 February, 2018.
Rafiki wa Rais wa zamani wa Korea ya Kusini Choi Soon Sil.



Rafiki wa aliyekuwa rais wa Korea Kusini, Park Guen Hye, ambaye aliondolewa madarakani kuhusiana na kashfa ya ufisadi, amehukumiwa kifungo cha miaka 20.

Choi Soon Sil alipewa adhabu hiyo na mahakama ya wilaya mjini Seoul, baada ya kukutwa na hatia ya rushwa, na kutumia madaraka kuwatisha watu.

Shirika la habari la Yonhap limesema kuwa kwa kutumia urafiki wake na Park Guen Hye na makampuni makubwa ya biashara kama Samsung, kukusanya michango kwa ajili ya wakfu aliouanzisha.

Mbali na kifungo gerezani, Choi pia ameamuliwa na Mahakama kulipa faini ya dola milioni 17, na alikuwa tayari amepewa adhabu ya kifungo cha miaka mitatu, kwa kushawishi upendeleo kwa ajili ya binti yake.

CHOI SOON SIL, AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MAISHA KWA KASHFA ZA RUSHWA. CHOI SOON SIL, AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MAISHA KWA KASHFA ZA RUSHWA. Reviewed by safina radio on February 13, 2018 Rating: 5

No comments