ZIJLSTRA ATANGAZA KUJIUZULU WADHIFA WAKE HAPO JANA KUTOKANA NA KUTOKUHUDHURIA MKUTANO WA RAIS.
AMSTERDAM.
Taarifa ya Habari saa 01:00 mchana, 14 February, 2018.
![]() |
Halbe Zijlstra, Waziri wa Mambo ya kigeni wa Uholanzi. |
Waziri wa Mambo ya kigeni wa Uholanzi,
Halbe Zijlstra ametangaza kujiuzulu wadhifa wake hapo jana kufuatia ufichuzi
kwamba alidangaya kuhusu kuhudhuria mkutano ulioandaliwa na rais wa Urusi.
Waziri huyo amekabiliwa na ongezeko la
wito wa kumtaka kuachia madaraka kutoka upande wa upinzani baada ya kukiri siku
ya Jumatatu kwamba alisema uongo kuhusu kuwa mgeni katika mkutano ulioandaliwa
na Rais wa Urusi, Vladimir Putin muongo mmoja uliopita.
Waziri mdogo wa wizara hiyo nchini
Uholanzi Sigrid Kaag, aliyeongoza ujumbe wa Umoja wa Mataifa ulioharibu silaha
za sumu nchini Syria mwaka 2013, atachukua majukumu ya waziri Zijlstra hadi
hapo atakapotajwa waziri mwingine atakayeongoza wizara hiyo.
ZIJLSTRA ATANGAZA KUJIUZULU WADHIFA WAKE HAPO JANA KUTOKANA NA KUTOKUHUDHURIA MKUTANO WA RAIS.
Reviewed by safina radio
on
February 14, 2018
Rating:

No comments