KAMKET APENDEKEZA MSWADA BUNGENI UNALENGA KUBADILISHA MFUMO WA KATIBA.
NAIROBI.
Mbunge
wa chama cha KANU nchini Kenya Kassait Kamket, amependekeza mswada bungeni
unaolenga kubadilisha mfumo wa uongozi nchini humo kwa kuibadilisha Katiba.
![]() |
Mbunge wa chama cha KANU nchini Kenya Kassait Kamket. |
Habari
zinasema kuwa iwapo Mswada huo utakubaliwa na wabunge, ina maana kuwa Katiba
mpya ya Kenya iliyopatikana mwaka 2010, itafanyiwa mabadiliko makubwa.
Mbunge
huyo anapendekeza kuundwa kwa wadhifa wa Waziri Mkuu atakayekuwa na madaraka
makubwa lakini pia kuwepo kwa rais ambaye atakuwa ishara ya umoja wa kitaifa.
Iwapo
marekebisho hayo yatafanyika, bunge la pamoja, lile la kitaifa na Senate
litamchagua rais ambaye atakuwa na jukumu la kumteua Waziri Mkuu kutoka kwenye
chama chenye wabunge wengi bungeni.
Waziri
Mkuu atahudumu kwa muda wa miaka mitano kabla ya Uchaguzi mwingine kufanyika,
huku rais ambaye ni lazima awe na zaidi ya miaka 50, akihudumu kwa muhula mmoja
wa miaka saba.
Wanasiasa
wa upinzani na viongozi wa dini wamekuwa wakisema mfumo huu ndio utakaosaidia
kumaliza mvutano wa kihistoria wa kisiasa hasa kuhusu wadhifa wa urais.
KAMKET
KAMKET APENDEKEZA MSWADA BUNGENI UNALENGA KUBADILISHA MFUMO WA KATIBA.
Reviewed by safina radio
on
February 28, 2018
Rating:

No comments