SERIKALI IMESEMA TATIZO LA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA NCHINI LIMEKUWA KUBWA.


TAREHE O9 FEB 2018
Image result for PICHA YA MH.JENISTA MHAGAMA

Serikali imesema tatizo la matumizi ya dawa za kulevya hapa nchini limekuwa kubwa na kuathiri vijana wengi huku bangi ikiwa dawa inayotumika zaidi na mmea huo ukiwa unastaishwa kwa wingio katika mikoa ya Mara, Mbeya, Njombe, Morogoro, Arusha, Tanga, Kagera, na Iringa.

Hayo yamebainishwa mjini Dodoma na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge Mh. Jenista Muhagama wakati akizungumzia athari  za dawa  za kulevya nchini na uthibiti wake ambapo amesema tafiti zilizofanyika nchini mwaka 2014 zinaonesha watu kati ya laki mbili na elfu hamsini hadi laki tano wanatumia dawa za kulevya aina ya heroin.

Aidha, Waziri Muhagama amebainisha kuwa katika tafiti hiyo kati ya watu hao laki mbili na elfu hamsini hadi laki tano, watu wapatao elfu thelethini wanatumia dawa hiyo kwa njia ya kujidunga.

Hata hivyo, Kamishna wa Tiba na Kinga wa Mamlaka ya kudhibiti na Kupambana Madawa ya Kulevya Peter Mpisi amesema kuwa katika kipindi kifupi mamlaka hiyo imekuwa ikipokea watu wengi wanaohitaji msaada kwa ajili ya vijana waliokuwa wanatumia madawa ya kulevya kutokana na kudhibitiwa kwa matumizi yake.

Hata hivyo serikali itaendelea na ujenzi wa hospitali hiyo kulingana na upatikanaji wa fedha ili wananchi waweze kupata huduma.

SERIKALI IMESEMA TATIZO LA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA NCHINI LIMEKUWA KUBWA. SERIKALI IMESEMA TATIZO LA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA NCHINI LIMEKUWA KUBWA. Reviewed by safina radio on February 09, 2018 Rating: 5

No comments