Rais wa Venezuela Nicolas Maduro ameitisha uchaguzi mkuu wa mapema utakao ambatana na kura ya rais mnamo April 22 mwaka huu. Maduro amesema kuwa uchaguzi mkuu unapaswa kuhusisha bunge, halmashauri na mamlaka za manispaa ili kuhakikisha kuwa kunakuwepo mageuzi kamili.


CARACAS.

Rais wa Venezuela Nicolas Maduro ameitisha uchaguzi mkuu wa mapema utakao ambatana na kura ya rais mnamo April 22 mwaka huu.  
Maduro amesema kuwa uchaguzi mkuu unapaswa kuhusisha bunge, halmashauri na mamlaka za manispaa ili kuhakikisha kuwa kunakuwepo mageuzi kamili.



 Rais huyo amesema mabunge yote yenye nguvu yataamua ikiwa kufanyike uchaguzi wa bunge miaka miwili kabla ya ilivyopangwa.

 Ikiwa Venezuela itaendelea na uchaguzi mkuu, inaweza kuathiri udhibiti wa upinzani bungeni baada ya muungano mkuu wa upinzani kutangaza kususia uchaguzi wa rais mapema siku ya Jumatano.

Muungano huo unasema hauwezi kushiriki katika uchaguzi huo kama hakuna hakikisho kutoka kwa serikali kwamba uchaguzi huo utakuwa huru na wa haki.

 Muda mfupi baada ya tangazo hilo la upinzani, Maduro amesema uchaguzi utafanyika kama ulivyopangwa licha ya mazingira hayo.

Serikali ya Venezuela imejitahidi kukabiliana na mgogoro wa kiuchumi baada ya bei ya mafuta kushuka mwaka 2014.

Rais wa Venezuela Nicolas Maduro ameitisha uchaguzi mkuu wa mapema utakao ambatana na kura ya rais mnamo April 22 mwaka huu. Maduro amesema kuwa uchaguzi mkuu unapaswa kuhusisha bunge, halmashauri na mamlaka za manispaa ili kuhakikisha kuwa kunakuwepo mageuzi kamili.  Rais wa Venezuela Nicolas Maduro ameitisha uchaguzi mkuu wa mapema utakao ambatana na kura ya rais mnamo April 22 mwaka huu.    Maduro amesema kuwa uchaguzi mkuu unapaswa kuhusisha bunge, halmashauri na mamlaka za manispaa ili kuhakikisha kuwa kunakuwepo mageuzi kamili. Reviewed by safina radio on February 22, 2018 Rating: 5

No comments