MAJALIWA AAGIZA KUKAMATWA KWA DAKTARI WA KITUO CHA AFYA CHA MAHUTA MKOANI MTWARA KUTOKANA NA MALALAMIKO YA WANANCHI KUHUSU WIZI WA DAWA.
MTWARA.
Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh
Majaliwa Kassim Majaliwa ameagiza kukamatwa kwa Daktari wa kituo cha afya cha
Mahuta mkoani Mtwara kufuatia malalamiko ya wananchi yanayodai kuwa daktari
huyo amehusika na wizi wa dawa unaosababisha wananchi kukosa huduma hiyo.
![]() |
Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. |
Mh Majaliwa ametoa maagizo hayo katika mji mdogo wa
Mahuta baada ya wananchi wa eneo hilo kusimamisha msafara wake na kuomba
kutatuliwa kero hiyo.
Amesema kuwa serikali imeshapiga marufuku dawa
zinazopelekwa kwenye Zahanati na vituo vya afya kutumika kinyume cha
sheria,hivyo daktari huyo anapaswa kukamatwa na kurudisha dawa hizo na kisha
kuchukuliwa hatua za kinidhamu.
Ameongeza kuwa lengo la serikali ni kuboresha huduma
za afya kwa kutoa fedha kila mwaka kiasi cha shilingi milioni 120 katika kila
Halmashauri,ambapo ametoa wito kwa Halmashauri zote hapa nchini kuhakikisha
kuwa kila zahanati na kituo cha afya kinakuwa na dawa za kutosha.
MAJALIWA AAGIZA KUKAMATWA KWA DAKTARI WA KITUO CHA AFYA CHA MAHUTA MKOANI MTWARA KUTOKANA NA MALALAMIKO YA WANANCHI KUHUSU WIZI WA DAWA.
Reviewed by safina radio
on
February 28, 2018
Rating:

No comments