MAGUFULI ATOA MSAADA WA FEDHA WENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 18 KWA HOSPITALI YA MANYAMA NYAMA.
MARA.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John
Magufuli ametoa msaada wa vitanda ishirini na tano, magodoro ishirini na mashuka
hamsini vyote vikiwa na thamani ya fedha zaidi ya shilingi milioni 18 ili
kuimarisha upatikanaji wa tiba katika hospitali ya wilaya ya Bunda ya Manyama nyama.
![]() |
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli. |
Akikabidhi vifaa hivyo kwa niaba ya Rais Mbunge wa
Viti Maalum Mkoa wa Mara Agnes Methew ametoa wito kwa wataalamu wa afya wa
hospitali hiyo kutimiza wajibu wao wa kuhudumia wagonjwa.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri
ya Bunda Janeth Mayanja pamoja na Mganga mkuu wa Hospitali hiyo Dk. Nicodemas
Masosota wamesema kuwa vifaa hivyo vitasaidia kutoa mapungufu yaliyopo katika
hospitali hiyo.
Hospitali ya wilaya ya Bunda ya Manyamanyama kwa
kipindi kirefu imekuwa ikikimbiwa na wagonjwa kutokana na ukosefu wa vifaa tiba
pamoja na wataalamu wa afya ambapo wagonjwa wengi wanalazimika kusaka tiba
katika hospitali ya Bunda BBH.
MAGUFULI ATOA MSAADA WA FEDHA WENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 18 KWA HOSPITALI YA MANYAMA NYAMA.
Reviewed by safina radio
on
March 01, 2018
Rating:

No comments