MAJALIWA AWAAGIZA VIONGOZI WA WILAYA YA TANDAHIMBA KUTHIBITI ONGEZEKO LA MIMBA ZA UTOTONI.


MTWARA.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa amewaagiza viongozi wa wilaya ya Tandahimba Mkoani Mtwara kuhakikisha kuwa wanadhibiti ongezeko la mimba kwa wanafunzi.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo wakati akizungumza na watumishi na Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda huku akiongeza kuwa lazima viongozi hao wasimamie nidhamu kwa kuwasimamia watoto wa kike ili waendelee na masomo yao shuleni pamoja na kutaka kukamatwa na kuchukuliwa kwa hatua za kisheri  kwa wote wanaohusika na kusababisha ujauzito kwa wanafunzi.

Aidha, Waziri Mkuu amesema kuwa mwaka 2016 mimba za utotoni ziliongezeka kutoka idadi ya mimba kumi hadi  mimba ishirini ambapo ni idadi kubwa hivyo jamii inapoteza wanafunzi wengi wa kike japo kuwa kuna wawakilishi na wasimamizi wa wananchi ambao walitakiwa kuonesha utaifa kwanza.

Hali kadhalika, Mh. Majaliwa amebainisha kuwa kwa 2017 mimba ziliongezeka kutoka idadi ya mimba ishirini hadi kufikia idadi ya mimba hamsini na saba jambo linalopelekea kupoteza idadi kubwa ya wanafunzi wa kike.

Hata hivyo, Mh. Majaliwa ameonesha hali ya kukerwa na hatua zinazofanywa na viongozi wa wilaya hiyo hususani watumishi hasa Afisa elimu, Mkurugenzi pamoja na Mkuu wa Wilaya na Kamati yake ya Ulinzi na Usalama wakiwa hawachukui hatua zozote kuhusiana na suala hilo.

Katika Hatua Nyingine Waziri Mkuu Majaliwa ametoa wito kwa watumishi wa umma kuhakikisha kuwa wanatekeleza majukumu yao kwa uadilifu na kwa kufuata sheria.

MAJALIWA AWAAGIZA VIONGOZI WA WILAYA YA TANDAHIMBA KUTHIBITI ONGEZEKO LA MIMBA ZA UTOTONI. MAJALIWA AWAAGIZA VIONGOZI WA WILAYA YA TANDAHIMBA KUTHIBITI ONGEZEKO LA MIMBA ZA UTOTONI. Reviewed by safina radio on March 01, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.