NGWIRA ASEMA SERIKALI INAZINGATIA MAHITAJI YA MAKUNDI MAALUMU.


ARUSHA.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Bi Anna Ngwira amesema kuwa serikali ya awamu ya tano kupitia wizara ya Afya inazingatia mahitaji ya makundi maalum wakiwemo wazee na watoto hivyo ameziagiza halmashauri zote nchini kuangalia uwezekano wa kuwapatia wabibi wote Bima ya Afya.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Bi Anna Ngwira.

Ameyasema hayo leo wakati akifunga Kongamano la Kitaifa la Bibi Tanzania lililofanyika Mkoani hapa ambapo Bi.Ngrwira amesema kuwa   utoaji wa bima hizo utakuwa ni mchango muhimu wa serikali kwa kazi wanayoifanya akina bibi hao katika malezi ya kuwalea wajukuu ambao wameachiwa kuwalea kutokana na wazazi wao kufariki kwa sababu mbalimbali.

Amesema kuwa kutokana na kutokuwepo kwa malipo ya uzeeni kwa wazee hao amezitaka Halmashauri husika kuwapa kipaumbele  wabibi wanaolea watoto hao katika mgao wa fedha  kupitia miradi ya vijana na wanawake itokanayo na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya kila Halmashauri kama sheria inavyoelekeza.

Aidha amelitaka Shirika la MWEDO pamoja na wadau wote waandaaji wa kongamano hilo kufuatilia na kuhakikisha huduma hizo zinatolewa kwa akina mama na kwa wabibi sambamba na kufuatilia kila Halmashauri ambazo wanatoka wabibi hao ili kuwawezesha kuhudhuria makongamano kama hayo.

Awali akisoma risala kwa niaba ya wabibi waliohudhuria katika kongamano hilo Bibi Edisi Tarimo amesema kuwa wabibi ni nguzo ya Taifa la Tanzania hivyo wanahitaji malipo ya uzeeni kwa wazee wote,njia za usaidizi kwa ajili ya mikopo binafsi ya kibiashara, kuwalinda dhidi ya ukatili na unyanyasaji na ubaguzi.

NGWIRA ASEMA SERIKALI INAZINGATIA MAHITAJI YA MAKUNDI MAALUMU. NGWIRA ASEMA SERIKALI INAZINGATIA MAHITAJI YA MAKUNDI MAALUMU. Reviewed by safina radio on March 01, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.