WANAJESHI WANNE WA KULINDA AMANI WA UMOJA WA MATAIFA WAUAWA NA WENGINE WANNE KUJERUHIWA VIBAYA, MALI.


BAMAKO.
Wanajeshi wanne wa kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa wameuawa na wengine wanne kujeruhiwa vibaya katika mlipuko wa mgodi katikati mwa nchi ya Mali.
WANAJESHI WA UN WAFA  KWA MLIPUKO MALI.
Vyanzo vya kiusalama vimesema mlipuko huo ulitokea majira ya alasiri wakati gari lililokuwa limewabeba askari zaidi ya kumi wa umoja wa mataifa lilipokanyaga kitu kinachosadikiwa kuwa kilipuzi kati ya maeneo ya Boni na Douentza katika kanda ya Mopti, katikati mwa nchi hiyo.
Afisa wa jeshi la serikali ya Mali ameviambia vyombo vya habari kwamba janga hilo jipya limefanya idadi ya askari wa kikosi hicho cha kulinda amani ambao wamepoteza maisha nchini Mali tangu mwanzo wa mwaka huu kufikia nane.
Umoja wa mataifa umesema wanajeshi wake wamekuwa wakikabiliwa na hali ngumu ya kudhibiti mashambulizi ya aina hiyo, kwa kuwa hadi sasa imekuwa kama kitendawili kumtambua adui anayetekeleza aina hiyo ya mashambulizi kwa kutumia vilipuzi.




WANAJESHI WANNE WA KULINDA AMANI WA UMOJA WA MATAIFA WAUAWA NA WENGINE WANNE KUJERUHIWA VIBAYA, MALI. WANAJESHI WANNE WA KULINDA AMANI WA UMOJA WA MATAIFA WAUAWA NA WENGINE WANNE KUJERUHIWA VIBAYA, MALI. Reviewed by safina radio on March 01, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.