REX TILLERSON AWATAKA WASHIRIKA WA MAREKANI KUENDELEA NA VITA DHIDI IS


WASHINGTON.

Taarifa ya Habari 08:00 Usiku,13 February, 2018. 
Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Marekani, Rex Tillerson akizungumza jambo na washirika wa Marekani.

Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Marekani, Rex Tillerson, amewataka washirika wa Marekani kuendeleza vita dhidi ya kundi linalojiita Dola la Kiislamu - IS, akisema kumalizika kwa operesheni kabambe dhidi ya kundi hilo hakumaanishi kuwa limeshindwa kabisa.

Tillerson ameyasema hayo leo katika mkutano wa ngazi ya mawaziri unaoendelea katika mji mkuu wa Kuwait, kuhusu vita dhidi ya IS na ukarabati wa Iraq.

Waziri Tillerson amesema IS bado ni kitisho cha usalama kwa kanda, wa baadhi ya mataifa washirika, na kwa baadhi ya sehemu nyingine duniani.
Desemba mwaka uliopita, Iraq ilitangaza kulishinda kundi hilo la kijihadi, lakini bado linashikilia maeneo nchini Syria.

Mapambano dhidi ya kundi hilo yamepata changamoto kutokana na operesheni zinazoungwa mkono na Uturuki, kaskazini mwa Syria, dhidi ya makundi ya Wakurdi ambayo ni washirika wa Marekani.



REX TILLERSON AWATAKA WASHIRIKA WA MAREKANI KUENDELEA NA VITA DHIDI IS REX TILLERSON AWATAKA WASHIRIKA WA MAREKANI KUENDELEA NA VITA DHIDI IS Reviewed by safina radio on February 13, 2018 Rating: 5

No comments