WAZIRI MKUU MAJALIWA KASSIM MAJALIWA ATAKA MASHAMBA YALIYOHIFADHIWA KWA AJILI YA MALISHO KUPIMWA.


TAREHE 08-02-2018

Waziri mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Majaliwwa Kassim Majaliwa ametaka Mashamba yote yaliyohifadhiwa kwa ajili ya malisho ya mifugo yaliyokuwa yanashikiliwa na NARKO chini ya Wizara ya Kilimo, kupimwa katika vitalu vitakavyowezesha kujua idadi ya mifugo ili kuwaruhusu wafugaji kufuga katika maeneo hayo.  

Mh Majaliwa ameyasema hayo leo bungeni mjini Dodoma katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa waziri mkuu ambapo  alikuwa akijibu swali la mbunge wa Misenyi Balozi Deodoras Kamala aliyetaka kujua serikali itamaliza lini  migogoro kati ranchi za taifa na vijiji vinavyoizunguka ranchi hizo kutokana na serikali kuiundia kamati ya kushughulikia mgogoro huo.

Mh. Majaliwa amesema kuwa kutokana na wananchi wengi kuwa na mifugo mingi huku wakikosa maeneo ya malisho, serikali imetoa utaratibu wa mashamba yote ya ranchi za taifa-NARKO  yaliyohifadhiwa kwa ajili ya malisho ya mifugo yapimwe katika vitalu ili wananchi wenye mifugo wapate maeneo ya kulishia mifugo yao sambamba na kuondoa migongano kati ya wakulima na wafugaji vijijni.

Amesema kuwa Wizara ya mifugo iliunda tume kufanya uhakiki wa maeneo ya ranchi za taifa ili kutambua wamiliki wa vitalu hivyo vilivyopimwa, idadi ya mifugo inayotakiwa, na kufahamu kama mmiliki wa kitalu amepata eneo hilo kihalali au vinginevyo ili kuweza kujua idadi ya maeneo yaliyopo kwa ajili ya kuwapeleka wafugaji wakubwa kufuga katika maeneo yao.

WAZIRI MKUU MAJALIWA KASSIM MAJALIWA ATAKA MASHAMBA YALIYOHIFADHIWA KWA AJILI YA MALISHO KUPIMWA. WAZIRI MKUU MAJALIWA KASSIM MAJALIWA ATAKA MASHAMBA YALIYOHIFADHIWA KWA AJILI YA MALISHO KUPIMWA. Reviewed by safina radio on February 08, 2018 Rating: 5

No comments