MAKAMU WA RAIS WA TANZANIA MH. SAMIA SULUHU HASSAN AMEZITAKA HALMASHAURI NCHINI KUWATAMBUA WAFANYABIASHARA WADOGO.
TAREHE 13-02-2018
Makamu wa rais wa jamuhuri ya muungano
wa Tanzania Mh Samia Suluhu Hassan amezitaka halmashauri zote za wilaya hapa
nchini kuwatambua wafanyabiashara wadogo maarufu kama wamachinga na
kuwarasimisha ili wajulikane na kasha kulipa kodi kulingana na kipato chao.
Mh Suluhu ametoa agizo hilo wakati
akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja
vya Mwembe Togwa mjini Iringa ikiwa ni sehemu ya ziara yake mkoani humo.
Amesema kuwa halmashauri pamoja na
mikoa zinatakiwa kuwarasimisha wafanyabiashara hao sambamba na kuwatengea eneo
la kufanyia biashara zao litakalokuwa na miundombuinu yote ikiwemo vyoo pamoja
na kuwa na sheria zao ndogondogo.
Aidha katika hatua nyingine makamu wa
rais amewataka watendaji wa serikali kudhibiti uharibifu wa vyanzo vya maji na
kuwaondoa wananchi wanaofanya shughuli zao kwenye vyanzo hivyo ili kuunga mkono
juhudi za serikali za kuhifadhi rasilimali na kukuza utalii hapa nchini.
Hata hivyo makamu wa rais yuko katika
ziara ya siku tano mkoani Iringa ambapo pamoja na mambo mengine atatembelea na
kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo na kutatua changamoto mbalimbali za
wananchi.
MAKAMU WA RAIS WA TANZANIA MH. SAMIA SULUHU HASSAN AMEZITAKA HALMASHAURI NCHINI KUWATAMBUA WAFANYABIASHARA WADOGO.
Reviewed by safina radio
on
February 13, 2018
Rating:

No comments