WATU 77 WAMEUAWA NCHINI SYRIA.
TAREHE 20-02-2018
Mashambulizi makali
ya jeshi la Syria katika eneo linaloshikiliwa na waasi la Ghouta mashariki yamewaua
raia 77, hayo ni kwa mujibu wa shirika la uangalizi wa haki za binadamu, wakati
majeshi ya serikali yakionekana kujitayarisha kwa mashambulizi ya ardhini.
Mashambulizi hayo
yametokeawakati ambapo majeshi yanayounga mkono serikali yakitarajiwa pia
kuingia katika eneo la Kaskazini linalodhibitiwa na Wakurdi kwenye mkoa wa
Afrin, ili kukabiliana na mashambulizi ya Uturuki.
Ukiwa unashikiliwa na
waasi tangu 2012, Ghouta imekuwa ngome ya mwisho ya upinzani mjini Damascus na
rais Bashar al-Assad amepeleka wanajeshi katika jitihada za kuutwaa tena.
Shirika la uangalizi
wa haki za binadamu lenye makao yake makuu mjini London limesema watoto 20 ni
miongoni mwa raia 77 waliouawa.
Mkuu wa shirika hilo
Rami Abdel Rahman amesema serikali inashambulia kwa mabomu mashariki mwa Ghouta
kusafisha njia kwa ajili ya mashambulizi ya ardhini.
WATU 77 WAMEUAWA NCHINI SYRIA.
Reviewed by safina radio
on
February 20, 2018
Rating:

No comments