NAIBU WAZIRI TAMISEMI JOSEPH KAKUNDA AMEWATAKA WATUMISHI WA SERIKALI KUWAJIBIKA IPASAVYO

TAREHE 21-02-2018


Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Mh Joseph Kakunda amewataka watumishi wa Serikali  hasa walimu   kuwajibika ipasavyo ikiwa ni pamoja na kusimamia majukumu yao vizuri ili kuongeza ufaulu kwa wanafunzi.

Kakunda ametoa kauli hiyo  wakati akipokea  nyumba sita za walimu zilizojengwa na  shirika la ECLAT Development pamoja na Upendo association na kuweka jiwe la msingi katika bweni la wasichana  katika shule ya sekondari Emboreti Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara.

Amesema kuwa walimu wanapaswa kufahamu kuwa kazi ya kufundisha ndio mkataba waliosainiana na Serikali hivyo Serikali inawataka kutekeleza majukumu hayo kwa ufasaha .

Ameongeza kuwa katika mkoa wa Manyara waalimu hawafundishi watoto ipasavyo na kuwa wengi wao wanajishughulisha na shughuli zao binafsi za biashara na kilimo

Mh Kakunda amesema kuwa mpango wa elimu msingi bila malipo umeamsha ari na moyo wa wazazi na walezi wengi hasa vijijini kutaka kupeleka watoto wao shule na kusababisha changamoto nyingi ikiwemo  upungufu wa miundombinu,ambapo amewaomba wadau mbalimbali wa elimu kuungana na Serikali katika kutatua changamoto hizo zinazoikabili sekta ya elimu.

Kwa upande wake mkurugenzi wa ECLAT  foundation  Peter Toima  amesema elimu ndiyo ufunguo wa maisha  na ndicho chanzo cha maendeleo hivyo Serikali pekee haiwezi kufanya kila kitu na ndio maana wao kama ECLAT  wameamua kuisaidia .

NAIBU WAZIRI TAMISEMI JOSEPH KAKUNDA AMEWATAKA WATUMISHI WA SERIKALI KUWAJIBIKA IPASAVYO NAIBU WAZIRI TAMISEMI JOSEPH KAKUNDA AMEWATAKA WATUMISHI WA SERIKALI KUWAJIBIKA IPASAVYO Reviewed by safina radio on February 21, 2018 Rating: 5

No comments