CONGO YASEMA KUWA ITAWACHUKULIWA HATUA MAAFISA USALAMA WANAOWAUA WAANDAMANAJI KWA RISASI.
KINSHASA.
Serikali
ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imesema kuwa, itaendelea kuwachukulia hatua
maafisa wa usalama watakaobainika kuwaua waandamanaji kwa kuwapiga risasi.
![]() |
Mahakama ya Kijeshi YA Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. |
Kauli
ho imekuja baada ya Mahakama ya Kijeshi hapo jana kumfunga jela afisa wa Polisi
kifungo cha maisha jela kwa kumpiga risasi na kumuua mwandamanaji katika eneo
la Mbandaka siku ya Jumapili iliyopita.
Wanaharakati
kadhaa wa haki za binadamu huko Mbandaka wamesema wanasikitishwa na namna kesi
hiyo ilivyoendeshwa, wakisema kuwa ilikuwa na lengo la kulinda wahalifu halisi
wa mauaji hayo.
Hayo
yanajiri wakati ambapo polisi mjini Kisangani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya
Congo, ikisema kuwa imewaachilia huru Makasisi watatu wa Kanisa Katoliki
waliokamatwa siku ya Jumapili iliyopita, wakiongoza maandamano ya kumshinikiza
rais Joseph Kabila kujiuzulu.
Polisi
nchini DRC imekua ikilaumiwa kutumia nguvu za kupita kiasi kwa kutawanya
maandamano hayo.
CONGO YASEMA KUWA ITAWACHUKULIWA HATUA MAAFISA USALAMA WANAOWAUA WAANDAMANAJI KWA RISASI.
Reviewed by safina radio
on
February 28, 2018
Rating:

No comments