MKURUGENZI JIJI LA ARUSHA AWATAKA MADIWANI KUTOTUMIA LUGHA ZISIZOFAA


TAREHE 07-02-2018

Mkurugenzi wa halmashauri ya jiji la Arusha Athuman Kihamia amewataka waheshimiwa madiwani wa halmashauri hiyo kutotumia lugha zisizofaa wakati wa kushiriki vikao mbalimbali badala yake washirikiane kwa pamoja katika kutatua matatizo ya wananchi.

Kihamia ameyasema hayo katika kikao cha baraza la madiwani cha robo ya pili kwa mwaka 2017/18 ambapo amesema kuwa kwa bajeti ya halmashauri kwa mwaka ni shilingi bilioni 14.58 huku mishahara ya tumishi ikiwa ni shilingi bilioni 32.

Naye Kalist Lazaro Meya wa jiji la Arusha wamewataka madiwani hao kutimiza wajibu wao kama baraza ili kuweza kuyafikia malengo ya kuwaletea wananchi maendeleo .

Kwa upande wake diwani wa Kata ya Ngarenaro Issaya Doita akizungumza katika kikao hicho amesema kuwa kutokusainiwa kwa baadhi ya mikataba ya vibanda kunasababisha halmashauri hiyo kukosa mapato ya kutosha .

Awali kabla ya kuanza kwa baraza hilo madiwani wawili  ambao ni Gaudence Lyimo kutoka Kata ya Kimandolu na Fransis Mbise kutoka Kata ya Muriet waliapishwa mbele ya Hakimu Krisanta Chitanda kutoka Mahakama ya Hakimu mkazi Arusha baada ya kushinda katika uchaguzi mdogo wa madiwani uliofanyika mwishoni mwa mwaka jana.
MKURUGENZI JIJI LA ARUSHA AWATAKA MADIWANI KUTOTUMIA LUGHA ZISIZOFAA MKURUGENZI JIJI LA ARUSHA AWATAKA MADIWANI KUTOTUMIA LUGHA ZISIZOFAA Reviewed by safina radio on February 07, 2018 Rating: 5

No comments