JAJI MKUU PROFESA. IBRAHIM JUMA AWAAGIZA MAHAKIMU WOTE KUTOA NAKALA ZA HUKUMU.
TAREHE 27-02-2018
![]() |
JAJI MKUU WA TANZANIA PROF. IBRAHIM JUMA |
Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Juma amewaagiza
mahakimu wote nchini kutoa nakala za hukumu bure kwa wananchi ili kurahisisha
upatikanaji wa haki kwa walengwa.
Prof. Juma ametoa kauli hiyo mkoani Kigoma ambapo
amesema mahakimu hao watakapokutana na kikwazo chochote cha sheria, kanuni au
taratibu katika utekelezaji wa agizo hilo wampelekee mapendekezo.
Amesema kuwa kutokana na mradi wa Benki Kuu ya Dunia,
unawataka watimize jukumu hilo la kutoa nakala za hukumu bure kwa wananchi kwa
kuwa wananchi wengi wanakosa nakala hizo kutokanan na kushindwa kulipia .
Pia, amesema kuwa kwa kuongezeka kwa suala hilo
kutasaidia kwa kiasi kikubwa katika kuchangia upatikanaji wa haki pamoja na kuwataka
mahakimu wote nchini kufanya kazi kwa weledi.
Hata hivyo, amesema kuwa kama kanuni zinatatiza
wahakikishe kanuni hizo zinabadilishwa sambamba na kuhakikisha madai yaliyopo
wawasililishe kwa Mtendaji Mkuu wa Mahakama ili arudishe fedha hizo.
JAJI MKUU PROFESA. IBRAHIM JUMA AWAAGIZA MAHAKIMU WOTE KUTOA NAKALA ZA HUKUMU.
Reviewed by safina radio
on
February 27, 2018
Rating:

No comments