Serikali imesema kuwa itawachukulia hatua wazazi watakaobainika kuwaficha ndani watoto wenye ulemavu badala ya kuwapeleka shuleni kusoma.



MTWARA.

Serikali imesema kuwa itawachukulia hatua wazazi watakaobainika kuwaficha ndani watoto wenye ulemavu badala ya kuwapeleka shuleni kusoma.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Majaliwa Kassim Majaliwa

Hayo yamesemwa na waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Majaliwa Kassim Majaliwa alipokuwa akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kitangari wilayani Newala mkoani Mtwara ambapo amesema kuwa watoto wote wana haki sawa ya kupata elimu ambapo kwasasa serikali inaandaa mazingira kwa watoto wenye ulemavu ili waweze kupata elimu bora nchini.

Aidha, Waziri Mkuu amesema kuwa watoto hao wanapaswa kusomeshwa kwa kuwa ni viongozi wa baadae katika nyanja mbali mbali za uongozi kama Mawaziri na Wakuu wa Wilaya ndani serikali ya nchi hii.

Pia, amesema kuwa watoto hao wakisomeshwa watakuwa wachangiaji wazuri wa maendeleo ya nchi na wala si sehemu ya nchi huku akiwaagiza watendaji wa vijiji kuwachukulia hatua wazazi wanaowaficha watoto hao ndani kila mwaka.

Hali Kadhalika, Waziri Mkuu ameagiza kuwa kila mtoto mlemmavu atolewe na kupelekwa shule kwa sababu serikali inatoa fedha za kuwahudumia watoto hao wenye mahitaji maalumu katika Halmashauri za wilaya wanazotoka.

Hata hivyo, Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa amesema kuwa hakuna sababu ya mtoto mlemavu kuwekwa ndani.

Serikali imesema kuwa itawachukulia hatua wazazi watakaobainika kuwaficha ndani watoto wenye ulemavu badala ya kuwapeleka shuleni kusoma. Serikali imesema kuwa itawachukulia hatua wazazi watakaobainika kuwaficha ndani watoto wenye ulemavu badala ya kuwapeleka shuleni kusoma. Reviewed by safina radio on February 28, 2018 Rating: 5

No comments