RAIS WA AFRIKA KUSINI CYRIL RAMAPHOSA KUTEUA BARAZA LA MAWAZIRI
TAREHE 21-02-2018
Rais mpya wa Afrika Kusini,
Cyril Ramaphosa amesema sasa umewadia wakati wa kufanya mabadiliko katika
baraza la mawaziri huku kukiwa na tetesi kuhusu kuendelea au kutoendelea
kubakia Waziri wa Fedha, Malusi Nkanyezi Gigaga.
Akizungumza jana nchini humo
Ramaphosa amesema ni wakati wa kutekeleza maneno yake kivitendo na kutafakari
kuhusu baraza la mawaziri na masuala mengine.
Ramaphosa
aliapishwa kuwa Rais wa Afrika Kusini siku ya Alhamisi iliyopita baada ya
chama tawala ANC kumlazimisha Jacob Zuma kujiuzulu kutokana na kashfa
kadhaa zilizokuwa zikimuandama katika kipindi cha miaka tisa ya
utawala wake.
Wadadisi wa mambo
wanasema, Gigaba anapaswa kuchukua maamuzi mazito katika bajeti ili kujaza
pengo la upungufu wa pato na pia kukabiliana na nakisi ya bajeti sambamba na
kuwasilisha ramani ya kuboresha uchumi uliovurugika wa Afrika Kusini.
RAIS WA AFRIKA KUSINI CYRIL RAMAPHOSA KUTEUA BARAZA LA MAWAZIRI
Reviewed by safina radio
on
February 21, 2018
Rating:

No comments