MUIGAI AJIUZULU BAADA YA KUHUDUMU KATIKA SERIKALI YA KENYA KWA MIAKA 6.
![]() |
Profesa Githu Muigai |
Akizungumzia uamuzi
huo rais wa Kenya Uhuru Kenyata amesema kuwa amepokea kwa majuto uamuzi wa
mwanasheria mkuu Githu Muigai,na anamshukuru kwa huduma yake katika kipindi cha
miaka sita na nusu.
Kabla ya uteuzi wake
kuwa mwanasheria mkuu profesa Muigai alikuwa mmoja wa wamiliki wa kampuni ya
mawakili ya Mohammed Muigai na amekuwa mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa katika
kukabiliana na ubaguzi wa rangi.
Alikuwa mwanafunzi
katika chuo kikuu cha sheria cha Columbia mjini New York na kutoka 1984 alikuwa
mwanfunzi katika chuo cha kusomea uanasheria nchini Kenya.
Akiwa mshauri wa
serikali katika masuala ya kisheria, Githu Muigai atakumbukwa kwa kuleta sheria
za mageuzi katika timu ya uchaguzi nchini Kenya siku chache tu kabla ya
uchaguzi kufanyika.
Hata hivyo rais
Kenyata amemteua Jaji Paul Kiharara kuwa mwanasheria mkuu mpya wa Kenya.
MUIGAI AJIUZULU BAADA YA KUHUDUMU KATIKA SERIKALI YA KENYA KWA MIAKA 6.
Reviewed by safina radio
on
February 13, 2018
Rating:

No comments