WATU 23 WAMEUAWA KATIKA MASHAMBULIO YA ANGA NCHINI SYRIA
TAREHE 08-02-2018
Takriban raia 23 wameuawa hadi sasa katika mashambulio ya anga ya vikosi vya serikali nchini Syria katika eneo la mashariki mwa Ghota karibu na mji wa Damascus,kunakodaiwa kuwa ni ngome ya waasi.

Takriban raia 23 wameuawa hadi sasa katika mashambulio ya anga ya vikosi vya serikali nchini Syria katika eneo la mashariki mwa Ghota karibu na mji wa Damascus,kunakodaiwa kuwa ni ngome ya waasi.
Waangalizi wa haki za binadamu kutoka Uingereza waliopo katika maeneo
hayo wameelezea hali hiyo na madhara kwa raia kutokana na mashambulio hayo.
Umoja wa mataifa
umetoa wito kusitishwa kwa mapigano hayo mapema iwezekanavyo,ambapo hapo awali
majeshi ya Syria yalidai kuwa vikosi vya anga vya Israel vilishambulia ngome za
kijeshi zilizopo karibu na mji mkuu Damascus.
Hata hivyo zaidi ya
watu 130 hadi sasa wanahofiwa kufa tangu vikosi vya serikali ya Syria
vilipoanzisha mashambulizi ya anga siku ya jumatatu wiki hii.
WATU 23 WAMEUAWA KATIKA MASHAMBULIO YA ANGA NCHINI SYRIA
Reviewed by safina radio
on
February 08, 2018
Rating:
No comments