Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Waziri Mkuu Mstaafu Mh. Mizengo Kayanza Peter Pinda amesema kuwa Chuo hicho kwa sasa kimejipanga kuanzisha utaratibu wa kozi fupi zitakazo waandaa watumishi wa umma kutekeleza azma ya serikali ya awamu ya tano ya uchumi wa viwanda.


KAGERA.

Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Waziri Mkuu Mstaafu Mh. Mizengo Kayanza Peter Pinda amesema kuwa Chuo hicho kwa sasa kimejipanga kuanzisha utaratibu wa kozi fupi zitakazo waandaa watumishi wa umma kutekeleza azma ya serikali ya awamu ya tano ya uchumi wa viwanda.

Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Waziri Mkuu Mstaafu Mh. Mizengo Kayanza Peter Pinda.

Mh Pinda ameyasema hayo wakati akikagua maendeleo ya Tawi ya Chuo hicho Mjini Bukoba mkoani Kagera wakati akizungumza na watumishi pamoja na wanafunzi.

Waziri Pinda amesema kuwa serikali itashughulikia changamoto zinazokikabili chuo hicho kutokana na uwezo wa kifedha utakaokuwepo na kuanzisha kozi fupi zitakazo waandaa watumishi wa umma katika ujenzi wa taifa.

Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Tawi la Kagera kilianzishwa mwaka 2000 kikiwa na wanafunzi ishirini na saba ambapo mwaka 2018 kina wanafunzi mia tano kikiwa kimefanikiwa kuanzisha vituo vya mitihani  katika wilayaa za Ngara na Karagwe.









Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Waziri Mkuu Mstaafu Mh. Mizengo Kayanza Peter Pinda amesema kuwa Chuo hicho kwa sasa kimejipanga kuanzisha utaratibu wa kozi fupi zitakazo waandaa watumishi wa umma kutekeleza azma ya serikali ya awamu ya tano ya uchumi wa viwanda.  Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Waziri Mkuu Mstaafu Mh. Mizengo Kayanza Peter Pinda amesema kuwa Chuo hicho kwa sasa kimejipanga kuanzisha utaratibu wa kozi fupi zitakazo waandaa watumishi wa umma kutekeleza azma ya serikali ya awamu ya tano ya uchumi wa viwanda. Reviewed by safina radio on February 26, 2018 Rating: 5

No comments