WANANCHI BURUNDI WALAANI JINSI MCHAKATO WA ZOEZI LA UANDIKISHWAJI WA KUPIGA KURA YA MAONI YA KATIBA YA BURUNDI.


BUJUMBURA.


Kulingana na ripoti ya HRW , vijana wa chama tawala cha Cndd-Fdd Imbonerakure, walishiriki katika mauaji ya kikatili mkoani Cibitoke kati ya Desemba 30 na Januari 3.


Zoezi la kuandikisha wapiga kura kuelekea kura ya maoni kuhusu marekebisho ya katiba nchini Burundi limeripotiwa kuendeshwa kwa haraka huku raia wakilaani jinsi zoezi hilo linavyoendeshwa kimabavu.

Habari zinaeleza kuwa wapiga kura watakao andikishwa katika zoezi hilo watakuwa na fursa ya kupiga kura katika kura ya maoni kuhusu marekebisho ya katiba inayopangwa kufanyika mnamo mwezi Mei pamoja na uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka 2020.

Katika muda usiozidi wiki mbili kutolewa kwa zoezi hilo kuanzia tarehe 8 hadi 17 Februari,Tume ya uchaguzi imekiri kuridhishwa na idadi ya watu ambao wamesha jiandikisha.

Tume hiyo imesema hadi Februari 14 asilimia 58 ya wapiga kura waliotarajiwa walikuwa wamesajiliwa lakini upinzani,mashahidi na vyombo vya habari vya kujitegemea vimeendelea kurusha matangazo yao nchini Burundi vikishtumu kwamba raia wanalazimishwa kujiandikisha kwa nguvu na tayari wameanza kufanyiwa vitisho.

Hata baadhi ya raia kutoka mikoani nchini humo wamebainisha kwamba wanafanyiwa vitisho vya kuuawa na kulazimika kwenda kujiandikisha kabla ya zoezi hilo kuisha.

WANANCHI BURUNDI WALAANI JINSI MCHAKATO WA ZOEZI LA UANDIKISHWAJI WA KUPIGA KURA YA MAONI YA KATIBA YA BURUNDI. WANANCHI BURUNDI WALAANI JINSI MCHAKATO WA ZOEZI LA UANDIKISHWAJI WA KUPIGA KURA YA MAONI YA KATIBA YA BURUNDI. Reviewed by safina radio on February 16, 2018 Rating: 5

No comments