AL-SHABAAB YAUWA WALIMU WATATU KWA SHAMBULIZI ENEO LA GARISA, KAUNTI YA WAJIR,KENYA.
NAIROBI.
Washukiwa wa kundi la Al-shabaab wamewauwa
walimu watatu siku ya leo katika shambulio lililotekea katika eneo la garisa
kaunti ya wajir nchini Kenya.
Kamanda wa jeshi la polisi Stephen
Ngetich alfajiri ya leo amethibitisha shambulizi hilo nakusema kuwa licha ya
walimu hao watatu kuuawa mwalimu mmoja alijeruhiwa.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari
inashukiwa kuwa wanamgambo wa Al-shabaab wamehama kutoka upande wa mandera na
kuweka kambi yao katika eneo la Wajir ambapo wameendelea kufanya mashambulizi
mara kwa mara katika miezi ya hivi karibuni.
Februari 12 Polisi waliokota miili
mitatu inayosadikiwa kuwa ya wapiganaji wa Al-shabaab waliouawa mapema katika oparesheni
ya polisi ya kuzuia shambulizi la magaidi hao katika kambi ya polisi nchini
humo.
AL-SHABAAB YAUWA WALIMU WATATU KWA SHAMBULIZI ENEO LA GARISA, KAUNTI YA WAJIR,KENYA.
Reviewed by safina radio
on
February 16, 2018
Rating:

No comments