MPANGO ASEMA TANZANIA INA TAKRIBANI WA WAPATAO MILIONI 54.2
DAR-ES-SALAAM.
Waziri wa fedha na mipango Dr Philip Mpango amesema
kuwa Tanzania inakadiriwa kuwa na idadi ya watu wapatao milioni 54.2 huku
asilimia 50 wakiwa na umri chini ya miaka 18.
![]() |
Dr Philip Mpango Waziri wa fedha na mipango. |
Dr Mpango ametoa takwimu hizo leo jijini
Dar-es-salaam wakati akizindua ripoti ya makisio ya idadi ya watu Tanzania
ambapo amesema idadi hiyo inakadiriwa kufikia watu milioni 59.4 mwaka wa 2021na
ifikapo mwaka wa 2030 idadi ya watu itafikia milioni 77.5.
Amesema kuwa kwa kuzingatia matokeo ya sensa ya watu
na makazi ya mwaka 2012 inakadiriwa kuwa kila mwaka kuna ongezeko la wastani wa
watu wapatao milioni 1.6 hapa nchini na kwamba ongezeko hilo linatokana na
idadi kubwa ya vizazi vipatavyo milioni
2.0 ikilinganishwa na idadi ndogo ya vifo ambavyo ni takribani laki nne kwa
mwaka.
Waziri Mpango ameongeza kuwa utafiti wa mama na
mtoto wa mwaka 2015 /2016 unaonesha kuwa mwanamke wa Kitanzania anazaa watoto
watano katika maisha yake yote ya uzazi ambapo matokeo yake idadi ya watu hapa
nchini imeendelea kuongezeka na kuifanya Tanzania kuwa nchi ya sita katika bara
la Afrika kwa kuwa na idadi kubwa ya watu baada ya Nigeria,Ethiopia,Jamuhuri ya
kidemokrasia ya Kongo na Misri.
MPANGO ASEMA TANZANIA INA TAKRIBANI WA WAPATAO MILIONI 54.2
Reviewed by safina radio
on
February 28, 2018
Rating:

No comments