SARA APEWA SIKU 30 KUHAKIKISHA KUWA MIGOGORO YA ARDHI WILAYANI HANANG' INATATULIWA KWA HARAKA.
MANYARA.
Mkuu wa wilaya ya
Hanang’ Mkoani Manyara Bi Sarah Msafiri amepewa siku 30 kuhakikisha kuwa
anatatua na kuimaliza migogoro yote ya ardhi iliyopo ndani ya Wilaya yake
ambayo imekuwa ikikwamisha Shughuli za maendeleo.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara Bw Alexander Mnyeti. |
Agizo hilo lilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Manyara Bw Alexander Mnyeti wakati
alipokuwa akizungumza na watumishi,na taasisi mbalimbali wilayani Hanang’
ambapo amesema migogogro hiyo baina ya kata na kata ,vijiji na vijiji ndio
unaowaathiri wananchi hao kwa kutumia muda wao mwingi katika migogoro badala
ya kufanya shughuli za maendeleo.
Bw Mnyeti amesema kuwa kila anayesababisha migogoro ya ardhi anatakiwa kukamatwa na kuchukuliwa hatua kwani Serikali imekuwa ikitumia fedha nyingi pamoja na muda kutatua migogoro hiyo ambayo whuku wanaosababisha wakiachwa bila kuchukuliwa hatua yoyote kisheria
Awali akisoma risala kwa mkuu wa mkoa Mkuu huyo wa Wilaya amesema kwa kipindi cha mwaka 2017/18 kulikuwa na jumla ya migogoro 63 ambapo migogoro mingi imetokea baada ya kuanzishwa kwa vijiji vipya mwaka 2014 lakini mpaka sasa tayari migogoro 18 imeshatatuliwa.
Hata hivyo ametaja
sababu zingine zinazochangia Migogoro hiyokuwa ni pamoja na Mihtasari iliyounda
vijiji hivyo kutofautiana na Government Notice GN, Baadhi ya vijiji kuanzishwa
kwa kutumia nyaraka zenye mapungufu ikiwemo mihtasari ya mikutano mikuu, na
baadhi ya wawekezaji wa mashamba makubwa kutotumia maeneo yote waliyomilikishwa
kisheria.
SARA APEWA SIKU 30 KUHAKIKISHA KUWA MIGOGORO YA ARDHI WILAYANI HANANG' INATATULIWA KWA HARAKA.
Reviewed by safina radio
on
March 14, 2018
Rating:
No comments