RAIS MAGUFULI AZINDUA RELI YA KISASA, STANDARD GEORGE IHUMWA DODOMA.


DODOMA.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania Dk. John Pombe Magufuli amezindua jiwe la msingi la ujenzi wa reli ya kati ya mwendo kasi ya Standard George inayotoka Morogoro hadi Dodoma katika eneo la Ihumwa Mkoani Dodoma.

Image result for Dk. John Pombe Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania Dk. John Pombe Magufuli.
Akizungumza katika uzinduzi huo uliohudhuriwa na viongozi mbali mbali wa kiseikali wa ndani na nje nchi ambapo amesema kuwa mradi huo wa awamu ya pili unagharamiwa kwa fedha za watanzania kwa zaidi ya shilingi trilioni 7.

Aidha, amesema kuwa mradi huo unatarajiwa kuajiri watanzania zaidi ya elfu thelathini kuwa wafanyakazi wa kudumu na wafanyakazi elfu sita wasio wa kudumu katika kutekeleza mradi huo.

Pia, amesema kuwa serikali ya awamu ya tano imejibu suala la ajira kwa vitendo ambapo ameeleze miradi mbali mbali mikubwa iliyoanzishwa na serikali katika kuleta maendeleo ya nchi ikiwemo mradi wa umeme wa Stilllers George, usambazaji wa umeme vijijini- REA, na ujenzi wa Meli kubwa katika ziwa Victoria.

Hata hivyo, amewataka wananchi kuwa wazalendo katika kulipa kodi ili kuharakisha maendeleo ya nchi huku akiita Mamlaka ya Ukusanyaji Kodi ya Tanzania-TRA pamoja na kuhakikisha kuwa inatoa elimu kwa wananchi kwa ajili ya kuondoa tabia ya ukwepaji wa malipo ya kodi.    

RAIS MAGUFULI AZINDUA RELI YA KISASA, STANDARD GEORGE IHUMWA DODOMA. RAIS MAGUFULI AZINDUA RELI YA KISASA, STANDARD GEORGE IHUMWA DODOMA. Reviewed by safina radio on March 14, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.