HALMASHAURI ZOTE ZA MKOA WA SIMIYU ZAAGIZWA KUWATUMIA WATAALAM KUPIMA ARDHI.

TAREHE 05-01-2018










Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi  Mh Angela Mabula ameziagiza Halmashauri zote mkoani Simiyu kuwatumia wataalamu wa ardhi kupima maeneo ya makazi ili wamiliki wa maeneo hayo wapate hati za kudumu.

Mh Mabula ametoa agizo hilo wakati alipotembelea  ofisi ya ukaguzi wa ardhi mkoani humo ambayo itatumika  kuhudumia mikoa ya jirani ya Mara na Shinyanga ili kumaliza migogoro ya ardhi katika mikoa hiyo.

Aidha, Waziri Mabulu amesema  kuwa mchakato wa upimaji ardhi mkoani Simiyu haufanyiki kwa njia inayostahili hali inayosababisha zoezi hilo kuendelea kusuasua hivyo jitihada za lazima zinatakiwa kufanyika katika zoezi hilo.


Hata hivyo, Bi. Mabula amesema viwanja vya maeneo ya miji katika mkoa wa Simiyu pia havijapimwa hivyo ameutaka uongozi wa halmashauri hizo kutoa vipaumbele katika upimaji wa ardhi katika maeneo ya mijini.
HALMASHAURI ZOTE ZA MKOA WA SIMIYU ZAAGIZWA KUWATUMIA WATAALAM KUPIMA ARDHI. HALMASHAURI ZOTE ZA MKOA WA SIMIYU ZAAGIZWA KUWATUMIA WATAALAM KUPIMA ARDHI. Reviewed by safina radio on January 05, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.