WAKAZI WA WILAYA RUANGWA WATAKIWA KUJIUNGA NA ICHF.

TAREHE 02-01-2018


Waaziri Mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa amewataka wakazi wa Wilaya ya Ruangwa kujiuga na Mfuko wa Afya ya Jamii-ICHF ili waweze kumudu gharama za matibabu bila ya kulazimika kuwa na fedha taslimu.

Waziri Mkuu ametoa wito huo katika mkutano wa hadhara wakati akizungumza  na mamia ya wakazi wa Mji wa Ruangwa na vijiji vya jirani.

Aidha, Waziri Mkuu Majaliwa amesema kuwa serikali imepiga hatua ya uhamasishaji wa wananchi kutumia mfumo wa Bima ya Afya kwa watu wote ili kila mwananchi aweze kupata huduma ya afya hata asipokuwa na fedha taslimu.

Hali kadhalika, Mh. Majaliwa ameongeza kuwa Mfuko wa Bima ya Afya-ICHF ni Mfuko wa watu wote na huchangiwa mara moja kwa mwaka ambapo mnufaika hupata matibabu bure katika kipindi chote cha mwaka.


Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Andrea Chizue, amesema mpango wa kutoa kadi za bima ya afya kwa wazee utawasaidia kupata matibabu  bure.
WAKAZI WA WILAYA RUANGWA WATAKIWA KUJIUNGA NA ICHF. WAKAZI WA WILAYA RUANGWA WATAKIWA KUJIUNGA NA ICHF. Reviewed by safina radio on January 02, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.