VIONGOZI WA VYAMA VYA CDU NA SPD WANAENDELEA NA MAZUNGUMZO NCHINI UJERUMANI
TAREHE 12-01-2018
Viongozi wa vyama ndugu vya CDU/CSU na chama cha SPD wanaendelea na mkutano wao mjini Berlin kuangalia uwezekano wa kuanzisha mazungumzo juu ya kuunda serikali ya mseto.
Kansela Angela Merkel
amesema vyama hivyo bado vinakabiliwa na vizingiti virefu kwenye mazungumzo
hayo,ambapo baada ya mazungumzo ya zaidi ya saa 18 makubaliano bado
hayajafikiwa baina ya pande hizo.
Vyombo vya habari
vimeripoti kwamba mazungumzo hayo huenda yakaendelea hadi hii leo Ijumaa
tofauti na ilivyopangwa.
Kansela Merkel anafanya juhudi za kuunda
serikali mpya ili kuunusuru mustakabali wake wa kisiasa,ambapo alionya hapo awali kwamba mazungumzo yatakuwa
magumu.
Hata hivyo kiongozi wa chama SPD Martin Schulz pia
amezungumzia juu ya kuwepo vizingiti vikubwa kwenye mazungumzo hayo.
VIONGOZI WA VYAMA VYA CDU NA SPD WANAENDELEA NA MAZUNGUMZO NCHINI UJERUMANI
Reviewed by safina radio
on
January 12, 2018
Rating:

No comments