RAIS WA ZIMBABWE EMMERSON MNANGAGWA AMESEMA UCHAGUZI MKUU NCHINI HUMO UTAFANYIKA NDANI YA MIEZI MITANO IJAYO

TAREHE 19-01-2018

Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa  ametangaza kuwa, uchaguzi mkuu wa nchi hiyo utafanyika katika kipindi cha miezi minne au mitano ijayo.
Mnangagwa ambaye alishika wadhifa wa urais wa Zimbabwe mwezi uliopita baada ya jeshi na chama tawala Zanu-pf kumshinikiza Robert Mugabe aliyekuweko madarakani kwa muda kwa miaka 37 ajiuzulu amenukuliwa na vyombo vya habari akitangaza kwamba, nchi hiyo itaitisha uchaguzi mkuu miezi minne hadi mitano ijayo.
Rais Mnangagwa amesema kuwa, uchaguzi ujao wa Rais, Bunge na serikali za mitaa utafanyika katika mazingira huru na ya haki,ambapo rais huyo pia mwenye  umri wa miaka 75 anatazamiwa kugombea kiti cha urais kwa tiketi ya chama tawala cha ZANU-PF.
Wakati huo huo Bw Roy Bennett, kiongozi wa upinzani aliyekuwa akiishi uhamishoni  amefariki dunia katika ajali ya helikopta iliyotokea katika jimbo la New Mexico nchini Marekani.
Ajali hiyo ya kuanguka helikopta imewahusisha pia watu wengine wanne waliokuwa wamefuatana naye akiwemo mkewe na amefariki akiwa na umri wa miaka 60.
RAIS WA ZIMBABWE EMMERSON MNANGAGWA AMESEMA UCHAGUZI MKUU NCHINI HUMO UTAFANYIKA NDANI YA MIEZI MITANO IJAYO RAIS WA ZIMBABWE EMMERSON MNANGAGWA AMESEMA UCHAGUZI MKUU NCHINI HUMO UTAFANYIKA NDANI YA MIEZI MITANO IJAYO Reviewed by safina radio on January 19, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.