MAGUFULI AMTUMIA RAIS KENYATA SALAMU ZA RAMBIRAMBI.



02-01-2018



Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi rais wa Kenya Mh Uhuru Kenyatta kufuatia ajali ya barabarani iliyosababisha vifo vya watu 36 baada ya gari la abiria kugongana na lori katika barabara ya Nakuru –Eldoret nchini humo hapo siku ya jana.

Katika salamu hizo rais Magufuli amesema ajali hiyo imesababisha majonzi makubwa si tu kwa Wakenya bali kwa wananchi wote wa jumuiya ya Afrika Mashariki hivyo kwa niaba ya watanzania wote anampa pole rais Kenyata na wananchi wote wa Kenya.

Rais Magufuli amesema kuwa anaungana nao katika kipindi hiki kigumu cha majonzi na amewaombea majeruhi wote wapone haraka.


Hata hivyo ajali hiyo ilitokea jana majira ya saa tisa usiku,ambapo kamanda wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Rift Valley Bw Zero Arome alisema kuwa madereva wote wawili ni miongoni mwa waliofariki katika ajali hiyo.
MAGUFULI AMTUMIA RAIS KENYATA SALAMU ZA RAMBIRAMBI. MAGUFULI AMTUMIA RAIS KENYATA SALAMU ZA RAMBIRAMBI. Reviewed by safina radio on January 02, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.