WATAKAOBAINIKA KUFANYA SHUGHULI ZAO KATIKA BONDE LA OEVU MTO KILOMBERO KUSHTAKIWA.

TAREHE 03-01-2018

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dk. Steven Kebwe Steven amesema kuwa watu watakaobainika kufanya shughuli zao katika bonde oevu la mto Kilombero watashtakiwa chini ya sheria ya kuhujumu uchumi.

Dk. Kebwe ameyasema hayo wakati akitoa taarifa ya uharibifu wa bonde hilo kwa Naibu Waziri wa Mali Asili na Utalii Mh Japhet Hasunga na kusema  kuwa tayari watu 20 wameshakamatwa kwa tuhuma za kuvamia bonde hilo na wengine kufikishwa mahakamani.

Naye Mratibu wa Bonde Oevu la mto Kilombero Bw Heledi Fauzeri amesema kuwa waliokamatwa waliokamatwa wakifanya uharibifu ni pamoja na watu wenye mifugo na wakulima wenye matrekta ambao walitaka kulima katika bonde hilo.

Hali kadhalika, Bw. Fauzeri ameongeza kuwa eneo la bonde hilo oevu ni kubwa pamoja na mifugo wanaoingia  ukilinganisha na idadi ya askari waliopo katika ulinzi wa eneo hilo hawalimudu.


Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, amesema ni lazima jitihada zifanyike za kulilinda bonde hilo huku akiagiza wizara na idara zote kuwa na lugha moja katika kulinda rasilimali za taifa.  
WATAKAOBAINIKA KUFANYA SHUGHULI ZAO KATIKA BONDE LA OEVU MTO KILOMBERO KUSHTAKIWA. WATAKAOBAINIKA KUFANYA SHUGHULI ZAO KATIKA BONDE LA  OEVU MTO KILOMBERO KUSHTAKIWA. Reviewed by safina radio on January 03, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.