WAZIRI MKUU WA SOMALIA AWAFUKUZA MAWAZIRI WATATU.
TAREHE 05-01-2017
Waziri
Mkuu wa Somalia Hassan Ali Khaire amewafukuza kazi mawaziri wake watatu huku
serikali yake ikiwa inakabiliana na changamoto kutoka upande wa upinzani.
Khaire
ametangaza majina ya watu watakaopokea nyadhifa za Waziri wa Mambo ya Nje Yusuf
Garaad Omar na balozi wa zamani nchini Marekani Ahmed Isse Awad.
Waziri
mkuu huyo pia amembadilisha waziri wa
mambo ya ndani na biashara pamoja na waziri wa viwanda,ambapo Abdi Mohamed
Sabriye ameteuliwa kuwa waziri mpya wa
mambo ya ndani na Mohamed Abdi Hayr wizara ya biashara.
Upinzani
katika taifa hilo la Pembe ya Afrika, umekuwa ukiishutumu serikali kuhusu
matukio ya usalama ya hivi karibuni ukitaka kumuondoa madarakani waziri mkuu.
Kundi
la waasi la al-Shabab linadaiwa kuhusika na shambulizi lililotokea mwezi Oktoba
mwaka jana, lililoua watu wapatao 512.
WAZIRI MKUU WA SOMALIA AWAFUKUZA MAWAZIRI WATATU.
Reviewed by safina radio
on
January 05, 2018
Rating:

No comments