WAKULIMA WILAYANI SIMANJIRO WATAKIWA KUSHIRIKIANA NA WATAALAM WAO.
TAREHE 17-01-2018
Wakulima wa wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara wametakiwa kushirikiana na
watalaamu wao hasa wakati huu wanapoelekea katika msimu wa kilimo ili waweze
kulima mazao yatakayowaletea faida kiuchumi.
Hayo yameelezwa na afisa kilimo wilaya ya Simanjiro
mkoani Manyara Bw Losloky Cloudy wakati akizungumza na Redio Safina jinsi
wilaya hiyo ilivyojipanga kushirikiana na wadau mbalimbali wa kilimo katika
kuboresha sekta hiyo ambayo ndio uti wa mgongo kwa wananchi wengi.
Amesema kuwa katika halmashauri ya wilaya ya
Simanjiro wananchi wengi ni wakulima na katika msimu huu wa kilimo wao kama
wataalamu wamekuwa wakitoa elimu kwa wananchi mbalimbali ikiwemo namna bora ya
kuandaa mashamba,namna ya kuandaa mbegu bora pamoja na mbolea ya kupandia.
Bw Cloudy ameongeza kuwa,ili mkulima aweze kupata
mazao mengi na yanayoweza kumletea faida kiuchumi ni lazima afuate kanuni na
taratibu za kilimo zinazotolewa na wataalamu wa sekta hiyo kwani wakulima wengi
wamekuwa wakifanya kilimo cha mazoea.
Kwa upande wake mtaalamu wa kilimo katika wilaya
hiyo Bi Warid Amani amesema kuwa wao kama wataalamu wamekuwa wakitoa elimu ya
kilimo kwa wakulima ili kuhakikisha kuwa wanalima kilimo chenye tija hivyo ni
vyema wakulima wakafuata elimu na utaratibu wanaopewa na wataalamu wao.
WAKULIMA WILAYANI SIMANJIRO WATAKIWA KUSHIRIKIANA NA WATAALAM WAO.
Reviewed by safina radio
on
January 17, 2018
Rating:

No comments