RAIS WA ZANZIBAR DK. SHEIN AAHIDI KUBORESHA SEKTA YA AFYA.
TAREHE 12-01-2018
Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la
Mapinduzi Dr Ally Mohamed Shein amesema kuwa serikali yake itaendelea kuboresha
sekta ya afya kwenye upatikanaji wa dawa na vifaa vya matibabu kwa kuongeza
bajeti katika wizara hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019.
Dr Shein ameyasema hayo leo wakati akihutubia
wananchi wa Zanzibar katika maadhimisho ya miaka 54 ya Mapinduzi yaliyofanyika
katika viwanja vya Aman mjini humo na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali
akiwemo rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh John Pombe Magufuli
Amesema kuwa katika mwaka wa fedha wa 2018 bajeti ya
wizara ya afya itaongezeka na kufikia shilingi bilioni 12,kutoka shilingi bilioni 7
kwa mwka wa fedha wa 2017/2018 lengo likiwa ni kuboresha huduma bora kwa
wananchi wanaokwenda kutibiwa katika vituo vya afya na hospitali.
Aidha rais Shein ameongeza baadhi ya mafanikio
yaliyopatikana katika sekta ya afya ni pamoja na kupungua kwa vifo vya akina
mama wanaojifungua, ambapo vimepungua
kutoka vifo mia mbili thelathini na saba kwa mwaka wa 2016 hadi vifo mia moja
tisini na tano kwa mwaka wa 2017.
Kwa upande wa watoto wachanga vifo vimepungua kutoka
54 kati ya watoto efu moja kwa mwaka wa
2010/2011 hadi vifo 43 kwa mwaka wa 2016/2017 kati ya watoto elfu moja.
Hata hivyo sherehe hizo za Mapinduzi ya Zanzibar
zimehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo marais wastaafu,mawaziri wakuu
pamoja na viongozi wengine wa dini na kisiasa.
RAIS WA ZANZIBAR DK. SHEIN AAHIDI KUBORESHA SEKTA YA AFYA.
Reviewed by safina radio
on
January 12, 2018
Rating:

No comments